SEVILLA FC 5-4 SIMBA SC, Kikosi cha Simba Kilivyoingia Uwanjani



Subscribes:

TIMU ya #SevillaFC ya Hispania imefanikiwa kutwaa Kombe la #SportPesaChallenge baada ya kuwafunga wenyeji, #SimbaSC mabao 5-4 katika mchezo maalum wa kirafiki Uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam usiku wa MEI 23, 2019.

Lakini haukuwa ushindi mwepesi, kwani Sevilla waliomaliza nafasi ya sita kwenye La Liga msimu walilazimika kutoka nyuma kwa mabao 3-1 hadi mapumziko ili kushinda 5-4.

Nahodha wa klabu, John Raphael Bocco alianza kuifungia Simba SC dakika ya nane kabla ya mshambuliaji mwenzake, Mnyarwanda Meddie Kagere kufunga la pili dakika ya 14.

Instagram:
Sevilla ikazinduka na kupata bao lake la kwanza dakika ya 24 kupitia kwa Jesus Escudero, lakini mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania, Bocco akaifungia Simba SC bao la tatu dakika ya 32.
Sevilla ikakianza vyema kipindi cha pili baada ya kufanikiwa kupata bao la pili kupitia kwa Bryan Gil dakika ya 48, lakini kiungo Mzambia, Clatous Chama akaifungia Simba SC bao la nne dakika ya 61.
Sevilla wakacharuka kuanzia dakika ya 85 wakipata mabao matatu na kuibuka na ushindi huo, kabla ya kukabidhiwa Kombe na Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo, Dk. Harrisons Mwakyembe.

Alianza winga Mholanzi, Quincy Promes kufunga mabao mawili dakika ya 85 na 89 kabla ya Manuel Agudo Durán maarufu kama Nolito kufunga la ushindi dakika ya tano ya muda wa nyongeza baada ya kutimia dakika 90.

Pamoja na kuchapwa, Simba SC ikajifariji baada ya Nahodha wake, John Bocco kukabidhiwa tuzo ya Mchezaji Bora wa Mechi hiyo.

Kikosi cha Simba SC kilikuwa; Aishi Manila, Zana Coulibaly, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Pascal Wawa, Jonas Mkude/Muzamil Yassin, Emmanuel Okwi, Clatous Chama, John Bocco na Haruna Niyonzima/Hassan Dilunga.

Sevilla: Juan Soriano, Jesus Escudero, Simon Kuaer, Ever Banega, Quincy Promes, Roque Sema, Wissam Ben Yedder, Emmanuel Agudo Nolito na Franco Vazquez.
Facebook:

Twitter:

Camisetas Brasil Información de primera mano del primer equipo de fútbol del Barça. Noticias de Piqué, Ansu Fati, Pedri y todos tus jugadores favoritos.